Mpera ni mti wa matunda ya kitropiki yenye virutubishi vingi na hutumika sana matunda yake kama chakula na pamoja na mmea wake ikiwa ni matunda, majani na magome yake pia katika tiba asili.Hivyo kwa matumizi ya mmea huo hupatikana afueni katika maradhi mbalimbali.
1.Husaidia kuimarisha mfumo wa kinga na kulinda dhidi ya maambukizo na magonjwa.
2.Nyuzinyuzi kwenye mapera husaidia usagaji chakula vizuri na kuzuia tatizo la kuvimbiwa na kujaa kwa gesi tumboni.
3.Mapera husaidia kudhibiti viwango vya sukari kwenye damu, na kuifanya kuwafaa watu wenye kisukari.
4.Husaidia kupunguza shinikizo la damu, kupunguza viwango vya cholesterol, na kuboresha afya ya moyo kwa ujumla.
5.Mapera ni matunda bora kwa udhibiti wa uzito kutokana na uwepo wake wa nyuzinyuzi.
6.Husaidia kupunguza uvimbe mwilini na kupunguza hali kama vile ugonjwa wa yabisi.
7.Majani ya mpera husaidia uponyaji wa jeraha.
8.Majani na magome ya mpera hupunguza makali ya maumivu ya hedhi.
9.Majani ya mpera yamekuwa yakitumika kitamaduni kutibu magonjwa ya kupumua kama vile kikohozi, na mafua.
10.Majani ya mpera husaidia kudumisha usafi wa kinywa, kupunguza kuvimba kwa fizi, na kutibu vidonda vya mdomo.
11.Majani ya mpera husaidia katika kuzuia kuharisha au tumbo la kuharisha.
1.Chai ya Majani ya Mpera:- Tia majani ya mpera kiasi katika sufuria nauwache yachemke na kuweza kutumia maji yake kwa manufaa mbalimbali katika mwili,1x3 kikombe kidogo cha chai .
2.Majani ya mpera twanga na majimaji kidogo na kubandikwa katika ngozi yenye majeraha au sehemu ulipojikata .
3.Magome ya Mpera:Chukua kiasi cha magome ya mpera na uweze kuchemsha katika sufuria na maji yakichemka uweze kutumia maji yake 2x3 ndani ya wiki moja,1x3 kikombe kidogo cha chai .
Jumatatu, 24 Februari 2025
MPERA
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Uwa la jerusalem
UA LA JERUSALEM Ni mmea ambayo midogodogo kwa kawaida huwa hutoa mauwa ya pinki, meupe na zambarau. Zifuatazo ni faida za mti wa ...
POSTS
-
ZAMDA Mbegu za Zamda, au mbegu za ajwain, ni mbegu zinazotokana na mmea wa Thymol Zamda, ambao hutumiwa sana katika upishi na dawa za j...
-
Shabu Shabu,Ni madini yenye rangi nyeupe hujulikana kwa sifa yake ya kutibia katika tiba asili ambayo ipo katika mfumo wa vipandepa...
-
MKUYU Miti ya mikuyu ni aina ya mtini uliotokea Afrika na Mashariki ya Kati. Ni ya familia ya Moraceae na inajulikana kwa dari kubwa, inay...
-
MTUNDA DAMU Mtunda Damu,Ni mti unaozaa matunda ambayo hujulikani kama matunda damu, matunda hayo hujulikana kwa umbile lake do...
-
ZAFARANI Zafarani ni kiungo kinachopatikana kutoka kwenye utambi wa ua la Crocus sativus, ambalo hujulikana kama ua la Zafarani. Ni moja ...
-
MSONOBARI Msonobari ni aina ya mti wa kijani kibichi wa coniferous katika jenasi Pinus, unaomilikiwa na familia ya Pinaceae. Misonobari ina...
-
MTINI Mtini,Ni aina ya mmea wa maua katika familia ya mulberry(Moraceae). Asili yake ni Mashariki ya Kati na magharibi mwa Asia lakini pia...
-
MTIKI Mti wa mtiki(Tectona grandis )ni mti mgumu wa kitropic kutoka kusini mashariki mwa Asia, hasa India, Indonesia, Malaysia na Myanm...
-
Ginseng Ginseng,Ni mmea wa kudumu unaokua polepole ambao mizizi yake hutumiwa kama dawa katika tiba asili katika nchi mbalimbali kam...
-
KOTO Faida za Koto kuzizungumzia kwa Mara moja haiwezekani kutokana na upana wa Tiba yake pia na maelekezo yake , Koto ina faida nyingi sa...
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni